ZAMARADI ANOGEWA NA KUZAA MTOTO

Mtangazaji wa Kipindi cha Take One, kinachorushwa kupitia Clouds TV, Zamaradi Mketema ‘Zama’ amefunguka kuwa, ataongeza tena watoto kwani tangu amejifungua mtoto wa pili ameona nyumba imekuwa na raha sana.
Mtangazaji wa Kipindi cha Take One, kinachorushwa kupitia Clouds TV, Zamaradi Mketema ‘Zama’.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni, Zamaradi alisema, ameshangazwa na furaha iliyotawala kwake na mzazi mwenzake na kwamba siku si nyingi atabeba mimba nyingine mbili fasta.
“Yaani watoto ni furaha kubwa, mimi nitaongeza tena wawili wa haraharaka maana nimegundua kuna kitu kinaongezeka kila unapoongeza mtoto mwingine ndani ya nyumba ikiwa ni pamoja na baraka,” alisema Zamaradi.

No comments:

Post a Comment