Hujitahidi kuvumilia misukosuko hiyo ili kuhakikisha anapata mkate wa siku hiyo, ili kutunza familia yake nakuendelea kuheshimiwa na watoto hata majirani kama baba mwenye kujali.Ishu inakuja pale mwanaume anaporudi nyumbani akitegemea kupokewa na mke wake kwa furaha, bashasha ili zimpoze na uchovu wa kazi alionao, lakini hali huwa si kama anavyotegema zaidi ya kukutana na karaha kutoka kwa wanawake wao.
Wakati mwingine mwanaume hutoka kazini mapema ila kila akifikiria makelele na karaha za nyumbani, basi anaamua kukata kona kwenye baa ili angalau apoteza muda wa kurudi nyumbani akute mkewe amelala.
Kama ulikuwa hujui vimada kwa sehemu kubwa wanacheza na fursa, wanajua kuzitumia ipasavyo.
Udhaifu wako dhidi ya mumeo ndiyo mafanikio ya kimada, anachofanya yeye ni kutumia ule udhaifu wako uliomfanya mumeo akachepukia kwake, yawezekana umeifanya ndoa yako kuwa ya mazoea, humpetipeti tena mumeo kama zamani.
Haumfanyii mambo mazuri kama enzi za uchumba, umtumbui chunusi kama mlivyokuwa mnatongozana na badala yake umegeuka Manny Pacquiao au Mayweather ndani ya nyumba, badilika mama!
Tukutane wiki ijayo katika mada nyingine nzuri zaidi.
No comments:
Post a Comment