UNATEGEMEA KUOLEWA KARIBUNI? KAMA NDIO TUNISHA MISULI YA NDOA.

Kuolewa ni tendo jema. Ni jambo Jema, na kila apataye mke amepata kitu chema.

Kwa maana hiyo kwa haraka sana ninaweza kukuambia maana ya kuolewa ni kwamba wewe msichana umekuwa kitu chema.
Kabla hujaolewa huitwi mke, ni msichana  ama mwanamke,, lakini  unapoolewa  tu  unabadilika na kuwa na cheo cha mke.
Na MKE  NI KITU CHEMA.
Mahali pengine anasema,   .. mali  na  mashamba mtu hurithishwa na babaye,,  lakini mke mwema anatoka kwa Mungu.
Hii inanikumbusha jambo  katka uumbaji wa Mungu, Mungu alipoumba  Ulimwengu alikusa akisema iwe inakuwa, lakini alipofikia kwa mwanadamu AKAUMBA, haikuwa tena iwe,, ila aliumba. Lakini nazidi kufurahi kwa sababu naona thamani ya mke hapa. Najiuliza kwa nini Adamu hakuumbiwa  mama na baba??  uliwahi kujiuliza swali hili  wewe  mwanamke?
Maana yake ni kwamba, Mungu alipomuumba mwanamke alimuumba katika ukamilifu wa hali ya juu  kuwa mke. Na ndio maana akasema  MKE NI KITU CHEMA.. kisha MKE MTU HUPEWA NA MUNGU… hii ni kwa sababu Mungu alimuumba  Eva/ Hawa  peke yake kwa viwango  vya kuwa mke… kukamilika katika UMKE.
Hivyo  ni lazima  wewe msichana kabla hujaingia kwenye ndoa ujihakikishie kwamba  NI MKE KITU CHEMA NA UMETOKA KWA MUNGU.
Tunaposema mke kitu chema nini maana yake?
Maana yake ni kwamba, KITU KIZURI, KISICHO NAMAWAA, KILICHO NA ADABU, HESHIMA,UTII,, THAMANI, MVUTO, NA KILA SIFA NZURI… Hii ndiyo maana ya KITU CHEMA.
Kama utakubaliana na mimi kwamba Mke ni kitu Chema,, basi utanihakikishia kabisa wewe mwenyewe kwamba nichaguo sahihi la mumeo. Lakini pia lazima ukubali kwamba,, katika wengi aliowaona wewe ndiye uliyekuwa MWEMA AMA CHEMA KULIKO WOTE, Na ndio maana
” chema huvikwa pete”
Ingia kwa miguu yote ndani ya ndoa yako ukiamini hivyo,, yes, na ndivyo ilivyo na ndivyo ulivyo.
Wengi wakishaingia kwenye ndoa hujikuta wanabadilika na kuwa tofauti na maana halisi ya Chema/ Wema. Unajikuta unaanza kupata Ugojwa wa kichaa cha ndoa… rejea somo la tarehe 7March 2015…
Hapa hapa kwa blog hii ya bembelezahappy women.
Kichaa cha ugonjwa wa Ndoa kinamuanza mtu pale ambapo anashindwa kujiamini na kujikubali yeye ni kitu chema, ama yeye ni chaguo la mumewe… ukishakosea ama ukishapoteza kujiamini hapa ndipo sasa matatizo ya ndoa yanaanza.
Wengi ambao wako kwenye ndoa zao na wamedumu na kuwa na furaha kwenye ndoa,,, JAMBO AMBALO LIMEWASAIDIA SANA NI KUJIKUBALI WAO NI KITU CHEMA NA KUMANTAIN HALI YA WEMA KATIKA NDOA ZAO.
Mithali 31:11-12
Mke kitu chema anachofanya hapa ni kuhakikisha mume wake anamuamini.. na mume atakuamini tu pale endapo utamtendea mema wala si mabaya… na akishakuamini …WEWE NI JEMBE AMA KOMANDO WA NDOA… Hutakuwa na kitu cha kukushinda kwenye ndoa,, kwa vile sasa wewe na mumeo ni mwili mmoja.. Mnaambatana… Mtakuwa mwili mmoja….
Hatua ya kwanza ni kumuacha baba na mama…..
Hatua ya pili ni Kuambatana… ….
Hatua ya tatu… ni kuwa mwili mmoja……..
Huwezi kuambatana na mumeo kama hujaamua kuacha mengine…
Hivyo INGIA KWENYE NDOA YAKO UKIWA UMEMAANISHA KUAMBATANA NA MUMEO.. KUIAMBATA NDOA YAKO…
Ukifanikiwa katika hili eneo basi wewe utaweza kuiendesha ndoa yako… kwa sababu ya urahisi upatikanao kwenye … kuambatana na kuwa mwili mmoja… lakini je unamaanisha kuolewa kweli? Unamaanisha kuwa mke wa mumeo kweli? Unamaanisha kuambatana naye na kuacha kila kitu kweli? Unamaanisha kuwa mwili mmoja naye?
NINI KINAMVUTIA MUME? Ni kuona..
Umeacha yote nayeye sasa amekuwa sehemu ya maisha yako.
Kuona unaambatana naye..
Kuona mmekuwa mwili mmoja…
MOYO WA MUMEO UKISHAKUAMINI BASI… hutakaa useme..
1. Ndoa ndoano.
2. Wanaume wote ni mbwa.
KOMAA ,,,, Sasa sio msichana tena,, ni mke wa Fulani, mama…. Ni lazima ujue na uwe na uwezo wa kujiendesha mwenyewe na kuiendesha ndoa yako ama nyumba yako… Kila kinachofanyika kwako wewe ndiye mhusika wa kwanza kuhakikisha mambo yanakuwa shwari,,, Hemaya yako inakutegemea sana wewe katika kuijenga utakavyo…
Unaolewa na mtu ambaye ana mawazo yake, taratibu zake, tabia zake.. sasa ni lazima uhakikishe unakuwa kitu chema ili sasa mfaidiane,,, mfurahiane,,, majukumu yako ni mengi sasa..
Kwanza kuweza kumsoma mumeo na kujua hapendi nini na anapenda nini.
Kurekebisha tabia usizozipenda zitoke ili zibaki unazozipenda.
Kuchochea nguvu kwenye tabia uzipendezao ili zizidi kukupendeza zisiishe… HIZI NDIZO KAZI ZAKO SASA.
Na unapokuwa mvivu ama mzembe Ndoa itakushinda haraka sana na kuanza kuwa wale waimbaji wa ule wimbo wa Wanaume wote ni Mmbwa… lakini sio kweli… “ men are not dogs”
kwa nini wanaume wote sio mmbwa? hao hao ambao wanaachika kwenye ndoa zao  hujikuta wakiwa na mahusiano  na wanaume tena,,  je  hao wanaume wanaokuwa nao  tena ni mmbwa?
KOMAA … WEWE NI KITU CHEMA….
Ili uwe na ndoa yenye furaha na amani, ni lazima ujikite kwenye kujua wajibu wako na  kuufanya. Ni lazima ndoa yako uijenge kwenye misingi imara  ama nguzo  imara zifuatazo:
KUUJUA WAJIBU   A.
KUUJUA WAJIBU  B.
KUUJUA WAJIBU C.
Wajibu  hizo  ziko katika group la Nakufunda Tayari kwa Ndoa. katika face book. Huko tumeziongelea wazi wazi na kwa uelewa  zaidi na kujimwaga zaidi.

No comments:

Post a Comment