MGOMO WA MADEREVA WAMALIZIKA.....MABASI YAANZA KUONDOKA UBUNGO KUELEKEA MIKOANI

Mgomo  Wa  Madereva  Umemalizika  Mchana  huu  baada ya majadiliano ya muda mrefu na mkuu wa wilaya  ya  Kinondoni.

Akisoma  makubaliano  hayo  mbele  ya  wenzake, kiongozi wa madereva   amesema  kuwa  madai  yao  yatatatuliwa  ndani  ya  siku 7 kupitia  timu  ya  madereva iliyoundwa kushughulikia  madai  hayo.

Mabasi ya mikoani kutoka Ubungo sasa yameanza safari baada ya mgomo wa takriban siku 2.

Makubaliano yaliyofikiwa ni kuundwa kwa kamati ya madereva zaidi ya 8 watakaokutana na mkuu wa wilaya kuanzia kesho.


 Kamati iliyoundwa inatakiwa kujadili madai yao kwa muda usiozidi siku 7 kwa usimamizi wa mkuu wa wilaya Paul Makonda

No comments:

Post a Comment