KAJALA NIACHENI NA MAISHA YANGU

Staa mkali wa filamu za Kibongo, Kajala Masanja.
Imelda Mtema
KUFUATIA mashabiki kumlaumu kwa kitendo chake cha kuhudhuria shoo ya Zari All White Party, staa wa filamu Bongo, Kajala Masanja amefunguka kwa ukali kuwataka watu kumuacha na maisha yake kwa sababu hayawahusu.
Akipiga stori na gazeti hili, Kajala  alisema  amekuwa mvumilivu kwa muda mrefu lakini kitendo cha watu kutaka kumpangia nini cha kufanya au wapi pa kwenda, kimevuka mipaka maana hawajui alipotoka wala anakokwenda.
“Watu wanazidi sasa, wanataka kunipangia wapi pa kwenda na wapi siyo pa kwenda, kwani kwenda kwa Zari kuna tatizo gani,  kwa hiyo mtu akiwa na tofauti na Wema, kila mmoja lazima atofautiane na huyo mtu? hayo mambo ya  wapi jamani, watu wasinipangie  maisha ya kuishi,” alisema Kajala

No comments:

Post a Comment