PENZI LA NEY WA MITEGO LASABABISHA WASANII KUCHAPANA HADHARANI MCHANA KWEUPE TENA BAA

HII sasa kali! Wasanii wa sinema ndani ya Bongo Movies, Fatuma Ayubu `Bozi’ na Brenda Marembeka `Kunguru’ wametoa aibu ya mwaka baada ya kupigana kwenye baa tena mchana kweupe kwa kile kilichodaiwa walikuwa wakigombea mabwana ambao ni mastaa  wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’ huku Kasim Yusuf `Young D’ naye akitajwa.
Wasanii wa sinema ndani ya Bongo Movies, Fatuma Ayubu `Bozi’ na Brenda Marembeka `Kunguru’ wakiamuliziwa baada ya kuzichapa.
Sekeseke hilo la aina yake lilijiri Jumatatu iliyopita kwenye Baa ya Mawela iliyopo Sinza jijini Dar ambapo kwa mujibu wa shuhuda mmoja wa tukio hilo, Bozi alitangulia kufika mahali hapo na kuagiza kinywaji.
WALIFIKA TOFAUTI
“Baada ya muda yule mwenzake (Kunguru) akafika na kuanza kumrushia vijembe mwenzake kisha kummwagia kinywaji chake na kumvua wigi alilokuwa amevaa.“Yaani hawa wasanii siyo siri wanaidhalilisha tasnia. Yule mwenzake alipofika tu, bila hata salamu akaanza kumtupia maneno makali mwenzake huku akimtuhumu kwa nini alitembea na bwana wa rafiki yake ambaye ni Nay wa Mitego kisha akaanza  kumkunja.
WAUMBUANA
“Yule mwingine (Bozi) akapamba moto na yeye, akasimama na kumuwakia mwenzake akimwambia  alitembea na bwana wake ambaye ni Yuong D. Yaani wamesababisha watu kujazana na kusitisha shughuli zao,” alisema shuhuda huyo.

MENEJA APATA WAKATI MGUMU
Wakati maparazi wanafika eneo la tukio walimkuta mtu mmoja aliyetambulishwa kuwa ni meneja wa baa hiyo akiwa katikati kuwaamua wasanii hao na kuambiwa waondoke.

Wakitupiana maneno baada ya kuamuliziwa.
WAHUDUMU PIA WANENA
Mbali na meneja kuwataka waondoke, wahudumu wa baa hiyo maarufu nao walionekana kutofurahishwa na kitendo cha wasanii hao kuzichapa kwenye baa hiyo kiasi cha kuwabughudhi wateja. Waliwatolea matusi mazito ambayo hayaandikiki gazetini huku wakiwaambia siku wakiziona sura zao kwenye baa hiyo wataishia polisi.

WENYEWE SASA
Baadaye kwa njia ya simu, mapaparazi wetu waliwatafuta wasanii hao, kila mmoja kwa wakati wake na kuwahoji juu ya ugomvi wao uliosababisha kujaza watu baa ambapo kila mmoja alimtupia lawama mwenzake kwa usaliti.

BOZI
“Yule Kunguru kwa kipindi kirefu hatujaonana na wala hatuongei. Cha ajabu leo nimekaa zangu pale baa nastarehe, hata sijui alipotokea, kaja na kuanza kunichokonoa. Ukweli mimi niliwahi kuwa na uhusiano na Young D kabla yake, yeye akaiba namba kwenye simu yangu wakatongozana mpaka kuwa wapenzi na huenda wameshaachana, sasa sijui kimemuuma nini? Labda alijua angeolewa.”


Staa  wa Bongo Fleva, Emmanuel Elibariki ‘Nay wa Mitego’.
KUNGURU
 “Sitaki kumuongelea huyo mtu, hana maana yoyote nitampa ujiko tu. Yeye alijua rafiki yangu (hakumtaja jina) anatoka na Nay na yeye akajipeleka. Kiko wapi sasa? Mbona kaachwa! Tena ndiyo kwanza kaambulia kusambaziwa picha zake za utupu mitandaoni.

NAY, YOUNG D
Kwa upande wake, Young D alipotafutwa kwa simu na kuambiwa kuhusu wasanii hao aligoma kuwazungumzia. Nay yeye alipoulizwa alianza kwa kucheka, akasema: “Ha! Ha! Mimi sijawahi kuwasikia hao watu na siwajui kabisa labda kuna kitu wanakitafuta kutoka kwangu.”
JIUNGE NA GLOBAL BREAKING NEWS

No comments:

Post a Comment