KIMENUKA!
Mume wa muigizaji nyota wa filamu nchini, Halima Yahaya ‘Davina’,
Abdallah Shakoor ambaye amekuwa kimya tangu kuenea kwa madai ya mkewe
kutoka na staa mwenzake, Mike Sangu, hatimaye amefunguka kuhusu skendo
hiyo na kudai anafuatilia kila hatua ya wawili hao na hivi karibuni
atatoa msimamo wake.
Chanzo chetu makini kimeripoti kuwa wasiwasi wa mume huyo kwa mkewe
ulianza muda mrefu uliopita, hasa baada ya staa huyo kusafiri kuelekea
Iringa kwenye mazishi ya shangazi yake akiwa ameongozana na Mike,
kitendo kilichomkera sana.
Inadaiwa kuwa kutokana na madai hayo kuandikwa magazetini mara kwa
mara, yamesababisha familia ya mume kutaka kujua kinachoendelea baina ya
wawili hao waliofunga ndoa yao Kiislamu.Gazeti hili lilipomtafuta mume
wa staa huyo alisema anasikitishwa na kinachoendelea kwa kuwa alimpenda
sana mkewe, lakini uvumilivu wake umefikia mwisho, hasa kufuatia kashfa
zinazotajwa dhidi yake.
“Jamani hakuna mwanaume anayefurahia kashfa za mkewe gazetini,
hainiletei picha nzuri kwenye familia, tena yenye maadili ya kidini kama
yangu. Siwezi kushindana na Mike kama mke wangu haoni tatizo.“Mimi
mwenyewe ni mtoto wa mjini sana, lakini sioni sababu ya kulumbana au
kumfanyia kitu Mike, kwa nini nifanye hivyo kama Davina haoni tatizo?”
alihoji.
Kuelekea Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, mume huyo alisema endapo Davina
ataendelea na maisha aliyojichagulia, atalazimika kuoa mwanamke
mwingine.Davina alipotafutwa alisema: “Kiukweli mimi bado nampenda mume
wangu ila kama anaamua hivyo, sawa.”
No comments:
Post a Comment