AUNT ASEMA BILA CHETI CHA NDOA, SIMUACHI MOSE IYOBO

Staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel ambaye hivi karibuni alipata mtoto aitwaye ‘Cookie’ amesema kama kuna mwanamke ambaye ana cheti cha ndoa na Moses Iyobo ajitokeze la sivyo hawezi kumuacha.
Staa wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel.
Akizungumza na Ijumaa hivi karibuni, Aunt alisema alipokuwa mjamzito amekuwa akipewa vitisho vingi ikiwa ni pamoja na mwanamke kudai ameporwa mumewe huyo.
“Kuna watu wanapenda sana kuongea, sasa mimi nasema kama kuna mtu ambaye ana cheti cha ndoa aliyofunga na Iyobo aje tu kisha mimi nitamuachia, la sivyo siwezi kumuacha,” alisema Aunt.

No comments:

Post a Comment