RAY ATESWA NA PICHA ZAKE ZA UTUPU MTANDAONI

Supastaa kunako Bongo Muvi, Vincent Kigosi, ‘Ray’ anateswa na tuhuma anazopata kutokana na mtu asiyejulikana kufungua akaunti feki ya Facebook yenye jina la Ray kisha kuposti picha za utupu.
Supastaa kunako Bongo Muvi, Vincent Kigosi, ‘Ray’.
Akizungumza na paparazi wetu, Ray alisema kuwa japokuwa ametoa ufafanuzi kupitia mtandao wake wa Instagram kuhusu picha hizo na akaunti hiyo feki, anashangaa kuona watu wanamuandama na kukomalia kwamba yeye anahusika.
“Yaani hii ishu inaniumiza na nimetoa ufafanuzi lakini sieleweki, naomba niseme kwamba mimi ni mtu ambaye najiheshimu sana, siwezi kufanya kitu kama kile mashabiki zangu waelewe hivyo tu,” alisema Ray.

No comments:

Post a Comment