THEA ASEMA HANA MPENZI NA WALA HAHITAJI MAANA NI SHIDAA

Msanii wa kitambo katika tasnia ya filamu Bongo, Ndumbangu Mesayo ‘Thea’ amefungua kinywa kwa mara ya kwanza kuwa, hivi sasa hana  wala hahitaji kabisa mpenzi na hapendi kukumbuka chochote kilichopita katika maisha yake ya kimapenzi.
Msanii wa kitambo katika tasnia ya filamu Bongo, Ndumbangu Mesayo ‘Thea’.
Akizu ngumza na gazeti hili juzi Thea alisema, hakuna kitu ambacho hakipendi kama kukumbuka mahusiano yake ya kimapenzi yaliyopita kiasi kwamba hata jina la aliyekuwa mumewe (Mike Sangu) eti kalisahau.
“Yaani sasa hivi sina mtu na wala sihitaji kabisa, mara nyingi sipendagi kukumbuka kabisa historia ya nyuma, ndiyo maana huwezi kuamini hata ukiniuliza jina la aliyekuwa mume wangu sikumbuki kabisa,” alisema Thea.

No comments:

Post a Comment