SAKATA LA ADEBAYOR NA FAMILIA YAKE: ADEBAYOR KUMWAGA 'UBUYU' MWINGINE WA MDOGO WAKE ROTIMI

Adebayor ametupia picha hii Facebook na kuahidi kutoa sehemu ya 2 ya stori ya kaka yake Rotimi.
SAKATA la straika wa Klabu ya Tottenham ya nchini Uingereza, Emmanuel Adebayor na familia yake limechukua sura mpya ambapo staa huyo ameahidi kutoa sehemu ya pili ya stori 'ubuyu' mwingine kuhusu kaka yake mwingine aitwaye Rotimi Adebayor muda muafaka ukifika.

Adebayor ameahidi kutoa ubuyu huo ikiwa ni siku chache tangu aachie waraka wa kwanza kupitia ukurasa wa Facebook uliokuwa ukielezea mambo anayofanyiwa na familia yake mbali na fadhila nyingi alizowafanyia.
Katika waraka huo Adebayor alifunguka mambo mengi akielezea anavyoibeba familia yake ambayo inaonyesha kutobebeka na badala yake kumtupia lawama kuwa hana msaada wowote kwa familia hiyo.
Kusoma waraka wa kwanza ingia: HAPA
Baada ya waraka huo, dada yake aitwaye Lucia Adebayor aliibuka na kukanusha taarifa hizo akidai ni uongo mtupu. Lucia aliandika hivi: "Lipo wapi gari ulilodai kumnunulia mama....si ulilichukua....Nyumba unayodai ulimnunulia dada ni uongo mtupu... Simu unazodai Rotimi aliiba nao ni uongo....fedha siyo kila kitu ooooo...sisi wanafamilia hatukutaki tena fanya mambo yako na sisi tufanye yetu.... kuwa nazo leo si kigezo cha kuwa nazo pia kesho Mwenyezi Mungu akusamehe...uliwafukuza wapwa wako ndani ya nyumba yako saa 6 usiku....Alpha na Mallams zimekuharibia maisha yako. Unamhitaji Mungu.... Mungu pekee ndiye anayeweza kuokoa roho yako." aliandika Lucia ambaye Adebayor ndani ya waraka wake wa mwanzo alimuelezea kuwa amekuwa akiwaambia watu kwamba baba yake alimwambia ampeleke Ulaya japo yeye hakuona sababu ya kumleta dada yake huyo Ulaya maana kila mtu yupo huko kwa sababu flani.

Adebayor akiwa na mama yake mzazi.
Staa huyo ameandika kuwa stori hiyo ya Rotimi itakuwa sehemu ya pili baada ya waraka wa mwanzo na kaka yake huyo ndiye aliyemuelezea kwenye waraka wa kwanza kuwa alipokuwa Monaco, alifikiria kuwa na familia ya wanasoka, hivyo akaamua kumpeleka ili ajiunge na akademi ya soka huko Ufaransa japo ndani ya miezi michache, kati ya wachezaji 27, aliiba jumla ya simu 21.
Mwaka jana Novemba, Adebayor aliibuka na kuwatuhumu mama yake na dada yake kwa madai kuwa wanatumia uchawi kumharibia kazi yake ya soka huku akikanusha kuwa hakumfukuza mama yake huyo kwenye nyumba yake bali aliamua kuondoka mwenyewe.
Kusoma habari ya Adebayor kumtuhumu mama yake kwa uchawi ingia: HAPA

No comments:

Post a Comment