MTU
mmoja aliyetambulika kwa jina la Abdikadiri Opapa anasakwa na Jeshi
la Polisi Mkoa wa Kipolisi wa Temeke baada ya kumtorosha mtoto wa kambo
na kumtishia maisha mke wake.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni baada ya wanandoa hao kuhitilafiana na mwanaume huyo kumuiba mtoto wa kambo aitwaye Machunda Thomas (11), aliyemkuta kwa mkewe huyo na kwenda kumficha kusikojulikana.Mke wa mwanaume huyo, Mwanaisha Omari amedai kuwa mumewe ametoa masharti kwamba ili amrudishe mtoto huyo ampelekee shilingi 400,000, hata hivyo hakusema ni za nini.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwanaisha alidai kuwa mumewe huyo baada ya kumuiba na kumtorosha mtoto wake, amekuwa akimpa vitisho huku akisema pesa hizo zikicheleweshwa atamuua mtoto huyo.
“Mtoto aliyemtorosha sikuzaa naye alimkuta lakini wakati ananioa nilimwambia na akaniambia kuwa yeye ni mtu wa swala tano, hivyo nisiwe na wasiwasi naye,” alidai Mwanaisha.
Hata hivyo, alidai kuwa baada ya muda mwanaume huyo alibadilika akawa anampiga kila anaporudi nyumbani akiwa amekunywa pombe, hali ambayo alisema ilimchosha.Alisema baada ya kuona hali ya vitisho inazidi alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha Kizuiani, Mbagala na kufunguliwa jalada namba MBL/3345/2015 - KUTISHIA KUUA KWA MTANDAO.
Kuhusu kutoroshwa kwa mtoto wake amefunguliwa jalada namba MBL/RB/3200 / 2015- KUMTOROSHA MTOTO. Hata hivyo, wakati tunakwenda mitamboni imeelezwa kuwa mtoto huyo alikutwa kwa baba huyo wa kambo maeneo ya Manzese lakini bwana huyo hakupatikana hivyo anasakwa na polisi.
Tukio hilo lilitokea hivi karibuni baada ya wanandoa hao kuhitilafiana na mwanaume huyo kumuiba mtoto wa kambo aitwaye Machunda Thomas (11), aliyemkuta kwa mkewe huyo na kwenda kumficha kusikojulikana.Mke wa mwanaume huyo, Mwanaisha Omari amedai kuwa mumewe ametoa masharti kwamba ili amrudishe mtoto huyo ampelekee shilingi 400,000, hata hivyo hakusema ni za nini.
Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwanaisha alidai kuwa mumewe huyo baada ya kumuiba na kumtorosha mtoto wake, amekuwa akimpa vitisho huku akisema pesa hizo zikicheleweshwa atamuua mtoto huyo.
“Mtoto aliyemtorosha sikuzaa naye alimkuta lakini wakati ananioa nilimwambia na akaniambia kuwa yeye ni mtu wa swala tano, hivyo nisiwe na wasiwasi naye,” alidai Mwanaisha.
Hata hivyo, alidai kuwa baada ya muda mwanaume huyo alibadilika akawa anampiga kila anaporudi nyumbani akiwa amekunywa pombe, hali ambayo alisema ilimchosha.Alisema baada ya kuona hali ya vitisho inazidi alikwenda kutoa taarifa Kituo cha Polisi cha Kizuiani, Mbagala na kufunguliwa jalada namba MBL/3345/2015 - KUTISHIA KUUA KWA MTANDAO.
Kuhusu kutoroshwa kwa mtoto wake amefunguliwa jalada namba MBL/RB/3200 / 2015- KUMTOROSHA MTOTO. Hata hivyo, wakati tunakwenda mitamboni imeelezwa kuwa mtoto huyo alikutwa kwa baba huyo wa kambo maeneo ya Manzese lakini bwana huyo hakupatikana hivyo anasakwa na polisi.
No comments:
Post a Comment