WAPENZI JAMANI, MNAKULA GIZANI MNAMFICHA NANI?

Natamani kucheka kwa jicho unalonikata na huku ukijisemea moyoni mwako kuwa siku ukinitia mikononi utanipasha nipashike, wapiiii, wan’kula huu na hasara juu. Hivi wee mung’unya jeuri ya kutaka kunipasha umeipata wapi? Kwa taarifa yako tu, hicho ni  kiburi cha nazi kutaka kushindana na jiwe.
Jamani leo nataka nizungumzie raha ya kusafiri, siku zote watu wengi, wanaume kwa wanawake wanapenda kusafiri usiku tena kukiwa na giza totoro, kweli si kweli?
Basi nawaambia raha ya safari ni mchana au hata kama ni usiku mwangaza uwepo babuuu…shurti mtu upate fursa ya kuona kule uendako.
Utaujua mji, utaona mandhari yake na kufaidi kuliko kusafiri usiku au kukiwa na giza.
Ndiyo, watu wanalipenda giza hawajui kuwa giza  ni la mwizi au wachawi… maana hata kama kuna taa wanazima na kuamua kusafiri gizani mpaka wanafika mwisho.
Jamani hakuna raha katika safari ya giza hata kidogo, kwani ukisafiri kweupe utaiona safari mwanzo hadi mwisho pia, mtu unapata fursa ya kuujua mji vizuri.Umenielewa au nimekuacha umelewa? Kama haitoshi nataka nikwambie kwamba utamu wa chakula ukione kwa macho yako kikiwa kwenye sahani safi.
Hapo hata kijiko cha kulia nacho ukikishika kinatulia mkononi. Utayaona maandalizi yaliyoandaliwa mezani na kukufanya uwe na hamu ya chakula ambacho machoni kitaonekana kuwa ni kitamu na kitakupa hamu ya kula, bado upo?
Hata ukila chakula huku unakiona ukisindikizwa na chombezo la maneno matamu hakika hutachoka kukitafuna kwa madaha huku utamu ukinoga na chenyewe kikikata kona katika mwili wako.
Eeeeheee! Acha niseme miye kwani  nisiposema leo nitasema  lini?  Unadhani nitasema nikiwa ndani ya kaburi?
 Kawaida ya wanawake huwa tuna milio yetu wakati wa safari, huwa tunahema kwa mihemo yenye kuongeza mahanjamu pale safari inapokolea.

Jamani kwa kuwa mada ni ndefu, tuonane wiki ijayo kwa mwendelezo wake.

No comments:

Post a Comment